Ngoja nianze na story hii, kuna mtu mmoja alikuwa anauza vile vipulizo vya watoto. Kila siku alikuwa akivijaza upepo na kuvirusha juu angani. Katika vipulizo hivyo alivyokuwa anarusha angani vilikuwa vya rangi nyekundu, njano, blue na kijani.
Kila akirusha vipulizo hivyo angani, watoto wanakimbilia na kuvinunua.
Siku moja akiwa anafanya hivyo, mtoto mmoja alikuja nyuma yake na kumuuliza:
“Ukirusha kipulizo cheusi kitaruka angani kweli”
Yule baba akajibu
“Mwanangu, kinachosababisha vipulizo hivyo viruke angani si rangi yake bali kile kilicho ndani yake”
Naomba kuuliza, nini umetunza ndani yako?
Una imani kiasi gani kuhusu uwezekano wa wewe kufanikiwa?
Kinachoamua hatima ya maisha yako si mapito unayopitia kwa nje bali kile kilicho ndani yako.
    
    Ni mimi ndugu yako; Mwl Nicholaus Simon.
    Kiungo katika mwili wa kristo.
    Kwa msaada zaidi na ushauri. 
    Mawasiliano: +255 766 635 382
    pataufahamu@gmail.com

   Ubarikiwe sana Na nakuomba nisaidie kuishare kwa marafiki zako ili na wao wajifunze Neno la Mungu.

Axact

Axact

Vestibulum bibendum felis sit amet dolor auctor molestie. In dignissim eget nibh id dapibus. Fusce et suscipit orci. Aliquam sit amet urna lorem. Duis eu imperdiet nunc, non imperdiet libero.

Post A Comment:

0 comments: