Tutaangalia katika maeneo matatu.(a) Familia (b) Kanisa (c) Nchi
Wajibu ni hali ya kuwajibika juu ya jambo fulani kwa wakati sahihi. Yoshua 1:1-9
Ukiangalia yote haya asemayo Bwana na Mtumishi wake, Yoshua ambaye kwa sasa ni wewe.
Mstari wa 5.''Hapatakuwa na mtu yeyote atakayeweza kusimama mbele yako siku zote za maisha yako; kama nilivyo kuwa na Musa, ndivyo ndivyo nitakavyo kuwa na pamoja na wewe; sitakupungukia wala sitakuacha.'' Tambua wewe ni mtu wa thamani na pekee sana, katika hii dunia. Hakuna kama wewe, Mungu alivyo kuumba amekuumba kwa kipekee na kukuweka vitu ndani yako ambavyo vitakusaidia kufanikiwa katika hii dunia. Zaburi 139:14-18
Mstari wa 6.''Uwe hodari na moyo wa ushujaa, maana ni wewe utakayewarithisha watu hawa nchi hii niliyowaapia baba zao yakwamba nitawapa.'' Wewe ni hodari, hakuna binadamu yeyote katika hii dunia. anayeweza kukukosoa kwa kusema, huwezi kufanya jambo fulani kwasababu  yeye hajakuumba  na ajui uwezo uliopo ndani  yako. 
Tambua ulivyo umbwa Bwana alikuchagua kati ya mbegu za kiume milioni tano, Mungu amekuchagua wewe. 1kor 2:7-8,11.
Hakuna mtu anayeweza kumjua mwenzake zaidi ya Mungu peke yake.
Mstari wa 7 ''Uwe hodari tu na ushujaa mwingi, uangalie kutenda sawasawa na sheria yote aliyokuamuru Musa mtumishi wangu;usiiache, kwenda mkono, au wa kushoto, upate kufanikiwa sana kila uendako'' Unapo wajibika  sawasawa na mapenzi ya Mungu hakika LAZIMA UFANIKIWE.

UKIWA KAMA KIJANA WAJIBU WAKO NI NINI NDANI YA FAMILIA.
Mambo ya kuangalia ili uwajibike sawasawa na mapenzi ya Mungu.                                                                                                                                
 (i) Ijue hali ya Familia yako. –maskini au tajiri, kabila lenu  katika upande wa mila na desturi.
(ii) Ijua haiba  ya wazazi wako  na ndugu zako. Kama ni sanguine, melancholic, flegimatic na choleric.
(iii) Tambua mila na desturi  za jamii inayo wazunguka. mafamo, baadhi ya makabila ni wakali sana, pia makabila mengine ni waongeaji. Ukiyatambua haya naamini utajua  ni jinsi  gani ya kuishi vyema bila makwazo yeyote na utapata ufahamu wa kuwa msaada mkubwa wa kuwasaidia  ndugu zako.  Mfano: Yusuph aliwatambua  ndugu  zake na baadaye aliwasaidia. Mwanzo 37:1-5
MUHIMU: Hata kama utafanikiwa  heshimu wazazi wako na ndugu zako.
''Waheshimu baba yako na mama yako; amri hii ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi.'' Waefeso 6:2
Usilipe ubaya wowote anaye lipa ubaya ni Mungu mwenyewe,wakati wote kuwa mtu wa kusamehe. ,1petr 2:17, kut 20:12, mith 13:1.
Jambo la muhimu la kujua,jamii yako hukudharau kwasababu kugundua kilichopo ndani yako ni vigumu mno. ''Wakachukizwa naye. Yesu akawaambia , nabii hakosi kupata heshima, isipo kuwa katika nchi yake, na nyumbani mwake mwenyewe.'' Mathayo 13:57

    UKIWA  KAMA KIJANA WAJIBU WAKO NI NINI NDANI YA KANISA.
Kijana katika Biblia takatifu ameelezwa kama, ''Mtu awaye yote asiudharau ujana wako, bali uwe kielelezo kwao waaminio, katika usemi na mwenendo, na katika upendo na imani na usafi.''1Tim 4:12         
 Kama kijana usijidharau wewe ni wathamani sana jikubali mwenyewe.
   ''Jitahidi kujionyesha kuwa umekubaliwa na Mungu, mtenda kazi asiye na sababu ya kutahayari, ukitumia kwa halali neno la kweli.'' 2Tim 2:15

Tambua kwamba vijana ndio walio leta mapinduzi makubwa katika kanisa la kwanza.  
Mambo ya Muhimu ya kuyafahamu
  (i) Jikubali wewe binafsi. Usijizalau  na kuona huwezi kutumika. 2Tim 2:15 -16    
 Wewe ni mzuri  kwasababu Mungu ndiye aliye kuumba hivyo ulivyo.
Zingatia: kila asubuhi jiwekee ratiba ya kumshukuru Mungu kwa jinsi hivyo ulivyo. 

(ii) Acha mizaa kabisa.
 ''Heri mtu yule asiyekwenda katika shari la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.'' Zaburi 1:1.  
    
MUHIMU: Acha mizaa na jinsia tofauti kwasababu jinsia tofauti ni hasi na chanya pale zinapo kutana lazima matokeo yatokee.''Wala msimpe Ibilisi nafasi.'' Efe 4:27

ZINGATIA
: unapo luhusu mizaa katika maisha yako, shetani hupata nafasi ndani ya moyo  wako.    
''Wala si ajabu, Maana shetani mwenyewe hujigeuza  awe mfano wa malaika wa nuru.''2kor 11:14

 (iii) jigundue uwezo wako binafsi katika mwili wa kristo
 Katika huduma tano zilizopo ndani ya kanisa jitahidi kujua  upo kwenye nafasi gani.
Je, wewe ni mchungaji, mwalimu, mwinjilisti, mtume na nabii. Pia jambo lingine la msingi la kifahamu ni kwamba kuna karama za Roho Mtakatifu zipo Tisa. 1kor 12:4

Nazo ni (i) KARAMA ZA UFUNUO. Ambapo ndani yake zinapatikana hizi tatu ;- Kunena, kutafsiri na Unabii.
         (ii) KARAMA ZA UFUNUO. Ambapo ndani yake zinapatikana hizi tatu ;- maarifa, neno la heekima na kupambanua roho. 
         (iii) KARAMA ZA  NGUVU.Ambapo ndani yake zinapatikana hizi tatu ;- Imani ,Uponyaji na matendo ya miujiza.
  Baada ya kupata ufahamu ju ya karama na huduma, tambua karama ni kifaa kinachowezesha huduma ikue . 
     MUHIMU: usibahatishe huduma yako.       
Kwahiyo kutimiza wajibu wako ndani ya kanisa Lazima utembee katika kusudi la Mungu.''Kwa kadiri ya kusudi la milele alilolikusudia katika kristo Yesu Bwanawetu.'Efe 3:11

     Vitu vya kuzingatia unapo chagua mahali pa kumwabudu Mungu ukiwa ugenini.
  • Ondoa mtizamo mgando wa kimadhehebu, tambua kanisa la kristo wote ni mwili mmoja.
  • Omba kwa Mungu akusaidie kukuongoza mahali sahihi. 

UKIWA KAMA KIJANA WAJIBU WAKO NI NINI NDANI YA NCHI.          
Tambua kwanza kuwa kanisa ndilo linalo ongoza nchi, kanisa likiharibika nchi nayo imeharibika.
Mungu anapo angalia nchi huangalia kanisa kwahiyo kama tulivyo angalia kama kijana, una umuhimu mkubwa sana ndani ya kanisa na nchi kiujumla.

Wajibu wako ni nini. 
(i)bidii katika masomoMith 4:13
(ii) bidii katika shughuli zako zote mfano, mashambani,maofisini, hii itakuwezesha kuwajibika vizuri katika Taifa .1Samweli 13:1,9-11.


MAMBO MAWILI YA MUHIMU KWA KIJANA
*    Kama kijana ombea Taifa kwa mzigo na ufanye kazi kwa nguvu, akili na moyo wako wote.
*    Kama kijana kila mwisho wa mwaka laziam ufanye tathimini ya mipango yako uliyo weka unapo anza mwaka.

Ni mimi ndugu yako; Mwl Nicholaus Simon.
Kiungo katika mwili wa kristo.
Kwa msaada zaidi na ushauri.
Mawasiliano: +255 766 635 382
pataufahamu@gmail.com


Ubarikiwe sana Na nakuomba nisaidie kuishare kwa marafiki zako ili na wao wajifunze Neno la Mungu.



                                                        

Axact

Axact

Vestibulum bibendum felis sit amet dolor auctor molestie. In dignissim eget nibh id dapibus. Fusce et suscipit orci. Aliquam sit amet urna lorem. Duis eu imperdiet nunc, non imperdiet libero.

Post A Comment:

0 comments: