AINA ZA MAOMBI YA KUFUNGA
----------------------------------------------------
Ushuhuda:
‘Mtumishi nashukuru sana kwa somo hili la maombi ya kufunga. Nataka nitoe ushuhuda halisi wa mimi mwenyewe jinsi maombi ya kufunga yalivyokata kiu ya dhambi ya uasherati. Mimi nilikuwa nimeokoka na nilikuwa nikianguka sana kwenye dhambi ya uzinzi pamoja na kwamba nimeokoka. Nilivyokaa na kuzingatia sana nikajuta ndani yangu. Nikachukua dhamira ya dhati nikaanza kufunga na kuomba mara 2 kwa wiki. Mtumishi tamaa yote ya dhambi ikamezwa na nguvu ya maombi ya kufunga”

-----------------------------------------------------
Tumsifu Yesu Kristo mwana wa Mungu.
Mwana wa Mungu, jana nilitoa utangulizi wa somo la maombi ya kufunga. Muhimu kujua kwamba kusudi la msingi la maombi ya kufunga ni kuutafuta uso wa Mungu ktk mambo fulani fulani.

Na pia ni vizuri kujua kwamba kufunga na kuomba ni kazi ngumu. Tunapaswa kuiruhusu neema na hekima ya Mungu kwa msaada wa Roho Mtakatifu vikuongoze kufunga na si matamanio yako binafsi. Tunaweza kufunga na kuomba iwapo tu tutakubali Roho Mtakatifu atufundishe na tuwe na utayari. Hakuna jambo mwanadamu atalifanya kwa uzuri wake pasipo neema ya Mungu na kujizoeza kwalo. Narudia neno hili kila leo kuna mazoezi ya kiroho ndugu zangu. Paulo amwambia Timotheo ‘jizoeze kupata utauwa’.

Tukitaka jambo lolote ktk kumtumikia Mungu tulifanye kwa uzuri wake lazima tujizoeze kulifanya. Kama ni kuhubiri injili, kufundisha, kuombea watu, kumtolea Bwana n.k. n.k. Ni lazima tujizoeze ndugu yangu haya mambo. Ni lazima tujizoeze kuishi maisha ya utakatifu Ni lazima tujizoeze kufunga na kuomba.
Tunapofunga na kuomba tunayatafuta mapenzi ya Mungu katika jambo Fulani. Bwana Yesu alitufundisha kuomba na akasema tuombapo tuombe ya kwamba “Mapenzi ya Mungu yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni” #Mathayo 6:10. Kwa hyo kusudi la kufunga na kuomba ni kuyatimiza mapenzi ya Mungu hapa duniani kama huko mbinguni! Kuyatimiza mapenzi katika hayo tunayoutafuta uso wa Mungu.


Kufunga na kuomba hakumfanyi Mungu ayabadilishe mapenzi yake. Hatufungi kuwaonyesha wanadamu ya kwamba sisi ni wa kiroho sana. Kwamba labda twamjua Mungu sana. Hapana. Tunayatafuta mapenzi ya Mungu maishani mwetu. Haijalishi umeokoka miaka mingi ilopita au hivi karibuni.

Tukumbuke maneno ambayo Mungu aliyasema ktk 2Nyak 7:14 “Ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao”

Kwa kufunga na kuomba tunamruhusu Roho Mtakatifu azihuishe nafsi zetu na kutufanya tuweze kusikia sauti ya Mungu na kumtii katika maisha yetu.

Kwa ujumla Tunafunga ili:

• Kuna watu wanafunga kwa sababu za kimwili kabisa. Kwamba miili yao imefika wakati inawapa shida. Matamanio ya mwili yameshindwa kuwasiliana vizuri na roho. Kuna nyakati tamaa za mwili zinakuwa kubwa na hivyo kwa kufunga na kuomba waweza kuutiisha mwili huu. Kwa vijana hasa, vyakula na vinywaji tunavyokula vinaleta shida wakati mwingine ndani ya mwili. Kwa kufunga unautiisha mwili na kuzinyamazisha tamaa hizo. Wengine wanafunga kwa ajili ya kuyatiisha mawazo. Bwana Yesu akasema mawazo ndiyo yamtiayo mtu unajisi. Kabla mtu hajafanya uasi Fulani huanza kujichafua katika mawazo yake. Ndani ya mawazo yake ataua, atamtukana mtu, atazini, ataiba yani atafanya kila lililo baya kabla hajalifanya katika ulimwengu wa kimwili. Rafiki yangu mmoja akasema ikiwa mwanadamu anaweza kupangilia mipango mbali mbali miovu hadi akaitimiza kwa nn asiweze kufanya hivyo hivyo kwa ajili ya Mungu? Kwa hyo wakati mwingine mtu anafunga kuyatiisha mawazo machafu ndani yake. Mawazo machafu hututia unajisi! Ndo maana mtume Paulo akasema “Basi, wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo, na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha Mungu” 2Kor 7:1

• Lakini kiroho tunafunga ili kuweka mahusiano yetu na Mungu vizuri rohoni. Ezra 8:21-23

“Ndipo nikaamuru kufunga, hapo penye mto Ahava, ili tupate kujinyenyekeza mbele za Mungu, na kutafuta kwake njia iliyonyoka, kwa ajili yetu sisi wenyewe, na kwa ajili ya watoto wetu, na kwa mali yetu yote. Maana naliona haya kumwomba mfalme kikosi cha askari na wapanda farasi, ili kutusaidia juu ya adui njiani; kwa maana tulikuwa tumesema na mfalme, tukinena, Mkono wa Mungu u juu ya watu wote wamtafutao, kuwatendea mema; bali uweza wake na ghadhabu yake ni kinyume cha wote wamwachao. Basi tukafunga, tukamsihi Mungu wetu kwa ajili ya hayo; naye akatutakabali”.


AINA YA MIFUNGO:

1. Mfungo kamili
Katika mfungo huu hakuna kula kabisa chakula kigumu bali waweza kunywa maji au kimiminika chochote cha kukusupport.
Siku ngapi waweza kufunga mfungo wa aina hii unategemea na neema na malengo yako katika mfungo huo. Wengine huenda siku moja, mbili, tatu, wiki, n.k n.k

2. Mfungo nusu

Mfungo nusu huanzia saa 12 asbh hadi saa 9 mchana au kuanzia jua linapoibuka hadi linapozama. Mfungo ambao madhehebu mengine wamewazoeza waumini wao kuufanya. Wengine wameweza kuufanya kila ijumaa. Madhehebu ambayo yamewazoesha watu wao kufunga angalau kila wiki mara moja wameweza kuwa na mafanikio makubwa sana katika kuzifungua nira na vifungo mbali mbali​

3. Mfungo wa Daniel
Daniel alifunga mifungo miwili ya aina yake;

• Katika Sura ya I Daniel alifunga alikula mboga mboga tu (Yaweza kuwa alikula mboga mboga na juisi Fulani Fulani)

• Katika sura ya 10 Daniel alifunga kwa siku 21 kwa kutokula chakula kitamu, wala nyama wala divai haikuingia kinywani mwake”​

Ngoja nikomee hapa kwa leo hadi wakati mwingine na Mungu akubariki sana na kama umependezwa na ujumbe huu hebu share na mwingine ili naye abarikiwe.

Nakushukuru sana wewe ambaye umekuwa ukibarikiwa na neno la Mungu ambalo tumekuwa tukijifunza pamoja kwenye huduma hii na umeona ni vema kuungana nasi kuwafikishia pia wengine injili (hasa walioko vijijini) kwa njia ya vipeperushi. Nawashukuru wote mnaoendelea kujitoa kwa ajili ya hili. Lengo letu ni kutengeneza vipeperushi angalau 5,000 kwa mwezi. Kipeperushi 1 ni tshs 250 tu. Kama unabarikiwa na neno ambalo tumekuwa tukishirikishana naamini utapenda pia watu walioko mazingira yasiyokuwa na Internet wafikiwe na injili hii kwa njia ya vipeperushi.

Ungana nasi kwenye huduma hii kwa kadri ya kufanikiwa kwako na Mungu akubariki. ‘Apandaye haba atavuna haba; apandaye kwa ukarimu atavuna kwa ukarimu. Kila mtu na atende kama alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima; maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu. Na Mungu aweza kuwajaza kila neema kwa wingi, ili ninyi, mkiwa na riziki za kila namna siku zote, mpate kuzidi sana katika kila tendo jema” #2KOR. 9:6-8. Hebu fanya kazi nasi kwa njia hii kwa kupenda. Ukichangia hata vipeperushi 2 (tshs 500 tu) kwa wiki au kwa mwezi waweza kuwafikishia injili watu zaidi ya 10. Utakuwa umeshiriki utume mkuu pamoja nasi. Basi changia kwa kadri ya kufanikiwa kwako.


YASIYOWEZEKANA KWA WANADAMU, KWA MUNGU YOTE YANAWEZEKANA

Kwa maombi | ushauri au unataka kumpokea Yesu akusamehe dhambi na abadilishe maisha yako basi ongea nami kwa tumia namba hii +255 712 204 937 |Kama unataka uwe unapokea mafundisho kila siku kwa Whatsapp +255 758 443 873 usiache kunipa majina yako|Unaweza pia kuwasiliana na mtenda kazi mwenzangu Mwinjilisti Emmanuel Jeremiah kwa simu namba +255 753 123 222 | Tuandikie pia kupitia
info@nenolauzima.org|  

Axact

Axact

Vestibulum bibendum felis sit amet dolor auctor molestie. In dignissim eget nibh id dapibus. Fusce et suscipit orci. Aliquam sit amet urna lorem. Duis eu imperdiet nunc, non imperdiet libero.

Post A Comment:

1 comments:

  1. Aisee Mtumishi Mungu wangu wa mbinguni akuponye Sana masomo yako kwa kwa kweli yanapiga hatua kwa nimepona Sana kupitia masomo yako

    JibuFuta