Karibu mpendwa mtu wa Mungu, Ujifunze somo zuri kutoka kwa mwl Fred. S. Mwabulambo, andaa tu moyo wako ili uweze kupokea kitu muda huu unapo soma.

Maandiko: 1 pet 1:14-16, Lawi 11:44, Waeb 12: 14 

Waebrania 12:4 (BHN) "Maana katika kupambana na dhambi, nyinyi hamjapigana mpaka kiasi cha kumwaga damu yenu." 


Mambo ya Walawi 11:44 "Kwa kuwa mimi ni Bwana, Mungu wenu; takaseni nafsi zenu basi; iweni watakatifu, kwa kuwa mimi ni Mtakatifu; wala msitie uchafu nafsi zenu kwa kitu kitambaacho cha aina yo yote, kiendacho juu ya nchi."

UTANGULIZI
A: Nini maana ya neno “Utakatifu”
          Ni ile hali ya kuwa safi mbele za Mungu, kumhofu yeye na kumwogopa yeye na kujitenga mbali na dhambi.
Neno “ Mtakatifu” lina maana mbili katika moja; Yaani kutengwa na dhambi kabisa na pili kuwekwa wakfu/ maalumu kwa ajili ya kazi/matumizi ya Bwana.
Hivyo: Utakatifu ni kutengwa na kujitenga na dhambi.
·         Tumeitiwa utakatifu, na lazima tuwe  watakatifu katika mwenendo wote (i) Mbele  ya watu (ii) sirini
B: Kipimo kikuu cha utakatifu
(ii) Yale yanayotendeka sirini.
                   Rum 2:16, Luka 12: 2, Kumb 29:29
Rum 2:16 "katika siku ile Mungu atakapozihukumu siri za wanadamu, sawasawa na injili yangu, kwa Kristo Yesu."
Luka 12:2  "Lakini hakuna neno lililositirika ambalo halitafunuliwa, wala lililofichwa ambalo halitajulikana." 
Kumbu 29:29 "Mambo ya siri ni ya Bwana, Mungu wetu; lakini mambo yaliyofunuliwa ni yetu sisi na watoto wetu milele, ili tuyafanye maneno yote ya sheria hii." 

·         Yanayotendeka sirini ndiyo kipimo kikuu cha utakatifu
·    Mungu anajua wanadamu wanaweza kufanya  mema machoni pa watu (Sirini wameshindwa, wanapokuwa peke yao).

Math 6:1"Angalieni msifanye wema wenu machoni pa watu, kusudi mtazamwe na wao; kwa maana mkifanya kama hayo, hampati thawabu kwa Baba yenu aliye mbinguni."

·         Hata nyakati za kwanza katika kanisa la karne ya kwanza, watu walitenda mambo ya aibu ndani ya kanisa kwa siri.
Efeso 5:12, Efeso 1:1 (Paulo anaongea na watakatifu). 

Efeso 1:1 "Paulo, mtume wa Kristo Yesu, kwa mapenzi ya Mungu; kwa watakatifu walioko [Efeso] wanaomwamini Kristo Yesu."
Efeso 5:12 "kwa kuwa yanayotendeka kwao kwa siri, ni aibu hata kuyanena."
·          Mtu anaweza kuongea na wewe na kwa tabasamu zuri usoni, lakini moyoni ni vita kali
Zaburi  55:21 "Kinywa chake ni laini kuliko siagi, Bali moyo wake ni vita. Maneno yake ni mororo kuliko mafuta, Bali hayo ni panga wazi."
  
·         Mwanadamu anafikiri Mungu ni kama mwanadamu mwenye ukomo katika kila jambo, Mungu anaona mpaka mawazo ya moyoni mwetu.
(Luka 6:7-8, Yoh  1:47-49)
Luka 6:7-8 "7 Na waandishi na Mafarisayo walikuwa wakimvizia, ili waone kwamba ataponya siku ya sabato; kusudi wapate neno la kumshitakia."
"8 Lakini yeye akayatambua mawazo yao, akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, Ondoka, simama katikati; akaondoka akasimama." 

·         Usimfiche Bwana chochote kile, yeye anaona yote
Isaya 29: 15, katika vifaa vya kiteknolojia tunatumia Password kuficha mambo yetu, Mungu hafichwi na password.

C: Jambo la kufanya ni hili
·         Uwe mtu mwenye hofu kama Daudi
Zaburi 139: 7-12, Mithali  28: 14
Mithali 28:14 14 "Mwanadamu mwenye kicho yu heri sikuzote; Bali mshupavu wa moyo ataangukia madhara."

·         Usifanye dhambi kwa kusudi  Hesabu 15:30-31, Waeb 10:26
·         Ungama na kutubu mbele za Bwana kwa maana ya kuacha kabisa
(Kiri kosa/confess).
                   Mithali 28: 13, 2pet 3:9
2petro 3:9 "Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba."
Mithali 28:13 "Afichaye dhambi zake hatafanikiwa; Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema." 
https://1.bp.blogspot.com/-5kP4R4fGlsE/XY8yqZWtxHI/AAAAAAAACGo/khGowEziAqwJP4mVTMcWjmyaQ2oMVH5gwCEwYBhgL/s320/1.jpg

D: kanuni ya uchaguzi ( 7 selection principles of what to do  and not to do)

Ili kujua kipi nifanye na kipi nisifanye ziko kanuni saba (7) zinazomwongoza mtu wa Mungu kuishi maisha matakatifu ya bila lawama katika ulimwengu huu wa uovu. Ni maswali 7 muhimu.

    1. Kabla ya kufanya jambo lolote inapaswa mtu ajiulize; je kama Yesu angekuwepo katika mwili pamoja nami akiniangalia; je ningefanya jambo hilo ninalotaka kufanya au je? angekubaliana na kitu hicho? kama jibu ni ndiyo, basi fanya na kama jibu siyo, basi usifanye kitu hicho, Yesu yupo anakuona katika kila usemalo, tabia na mwenendo wako wote uko wazi mbele zake. Kumbuka wewe siyo wa ulimwengu huu (Yoh 17:14-15)

   Yohana 17:14-15 "14 Mimi nimewapa neno lako; na ulimwengu umewachukia; kwa kuwa wao si wa ulimwengu, kama mimi nisivyo wa ulimwengu." "15 Mimi siombi kwamba uwatoe katika ulimwengu; bali uwalinde na yule mwovu." 

    2. Kanuni ya pili ni je kitu hicho kinasaidia kukuza imani yako katika Mungu? kama kitu hicho kinarudisha imani yako nyuma, hata kama kina Faida kiasi gani, lazima ukiache. Mfano Daniel na wenzake 1:12-16, walikataa chakula cha Mfalme, wakawa tayari kula mtama na maji tu.

   3. Tatu ni je? kitu hicho kinawakwaza wengine? Je, kina mfanya mwingine ashindwe kumuona Mungu katika maisha yake au kumrudisha nyuma aliyekwisha mjua Yesu? (Rum 14:21).
   Rum 14:21 "Ni vyema kutokula nyama wala kunywa divai wala kutenda neno lo lote ambalo kwa hilo ndugu yako hukwazwa."

    4. Nne ni je? kitu hicho kina haribu ushuhuda? (Luka 6:46). Kama kitu hicho kwa kukifanya watu watashindwa kumwona Yesu katika maisha.
     Luka 6:46 "Na kwa nini mnaniita, Bwana, Bwana, walakini hamyatendi nisemayo?"

   5. yao basi usifanye.Usifanye kitu chochote ambacho kitafanya watu watilie mashaka wokovu wako.

    6.    Ya tano, ni je? Kitu hicho kina haribu afya yako? au mwili wako?
 (1 Kor 3:16-17, 6:19). Biblia inasema wewe si mali yako mwenyewe (You are not of your own). Mwili wako ni hekalu la Mungu, hivyo ukiliharibu, Mungu atakuharibu wewe. Mabadiliko yoyote dhidi ya asili ya uumbaji wa Mungu hayakubaliki.Kumbuka Mungu alifurahia kazi yake ya uumbaji (Mwanzo 1:31).
Mwanzo 1:31 "Mungu akaona kila kitu alichokifanya, na tazama, ni chema sana. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya sita." 

   7.  Kanuni ya sita, ni je? ni cha lazima? (Isaya 55:2)je, kitu ninachotaka kufanya ni cha lazima? Kuna vitu vingine siyo lazima na havina umuhimu na ukilazimisha kuvifanya vitaleta matatizo, utatenda dhambi; subiri wakati wa Mungu. Mahitaji ya lazima ni chakula, malazi na mavazi ( 1 Tim 6: 7-8).
    1Timotheo 6:7-8 
"7 Kwa maana hatukuja na kitu duniani, tena hatuwezi kutoka na kitu;"
"8 ila tukiwa na chakula na nguo tutaridhika na vitu hivyo." 

   8.   Mwisho ni je? kitu hicho kitageuka kuwa Bwana wako? au kitakufanya kuwa mtumwa? (Rumi 6: 16, Yak 1:15) jihadhari sana na vitu ambavyo baadae vitakuwa Bwana na kukufanya kuwa mtumwa. Achana navyo vinginevyo utaharibu ukristo wako.
    Rumi 6:16 "Hamjui ya kuwa kwake yeye ambaye mnajitoa nafsi zenu kuwa watumwa wake katika kumtii, mmekuwa watumwa wake yule mnayemtii, kwamba ni utumishi wa dhambi uletao mauti, au kwamba ni utumishi wa utii uletao haki."
     Yakobo 1:15 "Halafu ile tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi, na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti." 

    Ni mimi ndugu yako; Mwl Nicholaus Simon.
    Kiungo katika mwili wa kristo.
    Kwa msaada zaidi na ushauri. 
    Mawasiliano: +255 766 635 382
    pataufahamu@gmail.com

    Ubarikiwe sana Na nakuomba nisaidie kuishare kwa marafiki zako ili na wao wajifunze Neno la Mungu.


Axact

Axact

Vestibulum bibendum felis sit amet dolor auctor molestie. In dignissim eget nibh id dapibus. Fusce et suscipit orci. Aliquam sit amet urna lorem. Duis eu imperdiet nunc, non imperdiet libero.

Post A Comment:

1 comments: