MICHAEL JACKSON
Wiki hii tuwe na tafakari hii Nimeinakili kutoka group la WhatsApp na kuiboresha kidogo. Simjui mwandishi ila ameandika kitu cha muhimu sana. Japo ningefurahi kumjua mwandishi ili nimpe zawadi yake. Nimeona na wadau wa Pata ufahamu Blog tuongeze ufahamu kupitia fuzo hili.
Michael Jackson alikuwa ni binadamu mwenye ndoto nyingi lakini Ndoto zake 2 kuu maishani zilikuwa ni:
1. Kwanza ni kuwa mwanamziki mkubwa zaidi duniani wa Pop.
2. Kuishi miaka 150.
Baada ya kuifanikisha ndoto yake ya kwanza kwa ufanisi mkubwa akiwa na miaka 25 tu aliamua kuanza kuwekeza kwenye ndoto yake ya pili ambayo kwa wakati huo ilikuwa ndiyo takwa lake kubwa.


Ili aweze kuishi miaka 150 (Karne moja na nusu) aliamua kufanya mambo yafuatayo:
1. Aliajiri madaktari binafsi 12 wa kumchunguza mwili wake wote hadi nywele na kucha kila siku.
2. Ilikuwa ni lazima chakula chake kipitie maabara kupimwa kabla hajala.
3. Aliwaajiri wataalamu 15 kufuatilia mazoezi, kazi na kila jambo alilofanya kila siku.
4. Alitengeneza kitanda maalumu kilichokuwa na uwezo wa kufanya 'regulation' ya hewa.
5. Watu 50 waliwekwa tayari kujitolea viungo vyao kama angepata dharura yoyote. 

Aliwalisha watu hao, aliwatunza na kuwalipa mshahara kila mwezi kwa kazi hiyo.
Baada ya kufanya hayo alikuwa na uhakika wa kuishi karne moja na nusu bila mashaka yoyote. Lakini June 25, mwaka 2009 akiwa na miaka 50 tu moyo wake ulizima ghafla na ndoto yake ikawa imefika mwisho.
Timu ya madaktari wake bingwa 12 haikuweza kuzuia pumzi yake isiondoke. Wale watu 50 waliowekwa 'standby' kumpa viungo hawakuweza kumsaidia. Akazima ghafla kama taa ya umeme iliyoishiwa luku.
Pamoja na juhudi za madaktari wengine kutoka Calfornia na Los Angeles hawakuweza pia kuokoa maisha yake. Mtu ambaye kwa miaka 25 alikuwa hawezi kunyanyua unyayo wake bila ushauri na ruhusa ya madaktari akawa kafika mwisho bila kutimiza ndoto yake ya kuishi miaka 150.
Safari ya mwisho ya Michael Jackson ilishuhudiwa moja kwa moja na zaidi ya watu milioni 3, rekodi ambayo haijavunjwa hadi sasa. Ndiye mtu aliyepata kuagwa na watu wengi zaidi katika historia ya dunia tangu enzi za Pontio Pilato.
Siku aliyofariki mitandao mikubwa ya Wikipedia, Twitter, Yahoo, AOL's instant messenger ilielemewa na mzigo wa watumiaji waliokuwa wakisaka taarifa za kifo hiki hadi ikaacha kufanya kazi. Google pia ilivunja historia ya matumizi yake kwa siku ile.
Michael Jackson alitaka kupambana na kifo lakini hakuweza hata kufikia nusu ya umri aliopenda kuuishi. Mtu aliyekuwa na uwezo wa kufanya lolote ili aweze kuishi umri autakao lakini alizima kama mshumaa upulizwapo na upepo. Biblia inasema ni yupi kwenu ambaye akijisumbua aweza kujiongeza kimo chake hata mkono mmoja? Hakuna. (Mathayo 6:27).
Ikiwa hatuwezi kuongeza hata kimo chetu basi hatuwezi kufanya lolote kuhusu hatma ya maisha yetu. Michael Jackson alifanya yote yaliyowezekana ili aishi miaka 150 lakini hakufika hata nusu ya umri huo. Lakini kuna mzee asiye na uhakika wa milo mitatu kule Tandahimba, Rombo, Ngara au Tukuyu ameishi umri mkubwa hata mara mbili ya Michael Jackson. Ni kwa neema tu.
Uhai na uzima tulionao ni zawadi kutoka kwa Mungu. Sio kwamba tunastahili kuliko wengine, hapana! Sio kwamba tumejitunza kuliko wengine, hapana! Ni kwa neema tu. Hata hatma ya maisha yetu ipo mikononi mwa MUNGU mwenyewe.
Hapa duniani hatuna mji udumuo bali sote twautafuta ule ujao. Ishi kwa upendo na amani na watu wote. Maandiko yanasema mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke siku zake za kuishi si nyingi (Ayubu 14:1). Tumuombe Mungu atuepushe na kiburi, atujaze upendo. Mungu atufundishe kuzihesabu siku zetu na kutujalia mwisho mwema.!
Ila Jambo moja la muhimu sana ambalo unaweza kulifanya likakupa uhakika wa Maisha yako ni
Kumwamini Yesu kristo kuwa Bwana na Mwokozi wa Maisha yako, hakika utakuwa upo kwenye eneo zuri san ahata pale utakapo ondoka hapa duniani utakuwa umejiandalia eneo salama la kufikia, Mwamini yesu leo upate uzima wa milele.
Fuatisha sala hii:

Nihurumie, Ee Mungu, kadiri ya fadhili zako; ufutilie mbali makosa yangu, kadiri ya wingi wa huruma yako. Unioshe kabisa hatia yangu; unisafishe dhambi yangu. Nakiri kabisa makosa yangu, daima naiona waziwazi dhambi yangu. Nimekukosea wewe peke yako, nimetenda yaliyo mabaya mbele yako. Uamuzi wako ni wa haki hukumu yako haina lawama. Mimi ni mkosefu tangu kuzaliwa kwangu, mwenye dhambi tangu tumboni mwa mama yangu. Naomba unifute jina langu kwenye kitabu cha hukumu na uandike jina loangu kwenye kitabu cha Uzima, kwa Jina la Yesu kristo….Amen 
                                                     Hongera kwa kuokoka 

    Ni mimi ndugu yako; Mwl Nicholaus Simon.
    Kiungo katika mwili wa kristo.
    Kwa msaada zaidi na ushauri. 
    Mawasiliano: +255 766 635 382
    pataufahamu@gmail.com

  Ubarikiwe sana Na nakuomba nisaidie kuishare kwa marafiki zako ili na wao wajifunze Neno la Mungu.
Axact

Axact

Vestibulum bibendum felis sit amet dolor auctor molestie. In dignissim eget nibh id dapibus. Fusce et suscipit orci. Aliquam sit amet urna lorem. Duis eu imperdiet nunc, non imperdiet libero.

Post A Comment:

0 comments: