Imani 

 Maandiko: Marko 9:19-23

19 Akawajibu, akasema, Enyi kizazi kisichoamini, nikae nanyi hata lini? Nichukuliane nanyi hata lini? Mleteni kwangu 20 Wakamleta kwake; hata alipomwona, mara yule pepo alimtia kifafa; naye akaanguka chini, akagaa-gaa, akitokwa na povu. 21 Akamwuliza babaye, Amepatwa na haya tangu lini? Akasema, Tangu utoto. 22 Na mara nyingi amemtupa katika moto, na katika maji, amwangamize; lakini ukiweza neno lo lote, utuhurumie, na kutusaidia. 23 Yesu akamwambia, Ukiweza! Yote yawezekana kwake aaminiye. 24 Mara babaye yule kijana akapaza sauti, akasema, Naamini, nisaidie kutokuamini kwangu.


Imani ya kweli katika Yesu ni msingi imara katika maisha ya kiroho. Ni jibu la mambo yote. Ni mkono unaochukua majawabu ya mahitaji yetu kutoka ulimwengu usioonekana na kuyafikisha kwenye ulimwengu wa mwili, tukaona kwa macho na kushika kwa mikono yetu.

Imani ni nini?
Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.
(Ebr 11:1)

Imani inakuthibitishia kuwa kitu unachokihitaji kimepatikana sasa wakati kinatarijiwa; imani inakiona:kitu halisi na kukikamata wakati hakipo.

Nchi ya Israeli ilikumbwa na ukame mbaya sana, ikatokea njaa kali, ikasababisha watu kula watoto wao, punda na mavi ya njiwa. Katika nyakati hizo za ukame nabii Elisha aliyekuwa na imani katika Mungu alitangaza kuwa kesho kutapatikana unga tele na nafaka mbalimbali. .Imani iliona mbali ikavuka mipaka ya ufahamu wa kibinadamu. Askari wa mfalme aliona kmwili Elisha aliona kiroho.
Elisha akasema, Lisikieni neno la Bwana; Bwana asema hivi, Kesho panapo saa hii, kipimo cha unga mzuri kitauzwa kwa shekeli, na vipimo viwili vya shayiri kwa shekeli, langoni pa Samaria (2Fal 7:1)
Kesho yake kweli yote yalitimia; soma (2Fal 7:1-20) Askari wa mfalme alikufa kwa kutokuamini.

Imani inazaliwa na inakua.
Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo. (Rum 10:17)
Imani ya kweli inazaliwa kwa kusikia Neno la Kristo. Imani inakua kila wakati inapotumika kuleta majibu ya mambo magumu. Yesu alifundisha somo la imani inayoleta matokeo.
(Mathayo 17:20) Yesu akawaambia, Kwa sababu ya upungufu wa imani yenu. Kwa maana, amini, nawaambia, Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, Ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu.

Imani inayoweza kuhamisha milima ya matatizo yako yote, inanza na kiasi cha punje ya haradali iliyo ndogo kuliko punje ya mchicha. Fahamu kuwa punje hiyo ikipandwa inaota na kukua hadi kuwa mti mkubwa. Na imani yako itakua kwa kadiri unavyoitumia kutatua matatizo yanayokukabili siku kwa siku.

Daudi alikuwa na ujasiri wa kukabiliana na Goliathi kwa sababu imani yake ilikua katika Bwana kwa kuwaua simba na dubu.

(1Sam17:36 ) Mtumishi wako alimwua simba na dubu pia; na huyu Mfilisti asiyetahiriwa atakuwa kama mmoja wao, kwa sababu amewatukana majeshi ya Mungu aliye hai.

Baba wa kijana tuliyemsoma hapo juu alimwomba Yesu kwa mashaka akisema, “lakini ukiweza neno lo lote, utuhurumie, na kutusaidia”. Bwana Yesu alimjibu kwa maneno yake , “Ukiweza! Yote yawezekana kwake aaminiye”. Yule baba alitambua haraka kosa lake akatubu na kuamini. Yesu akamponya mwanawe saa ileile.

Kizazi chetu tunafanana na baba huyo; tunafahamu kuwa Yesu anaponya, anaokoa na kutenda miujiza mingi. Inapokuja kwenye mahitaji yako wewe binafsi imani inapungua. JiulizeYesu amekufanyia nini? na unamtarajia akufanyie nini katika matatizo yako?  Je unaamini kweli anaweza? Je moyoni mwako mna mahangaiko na kutangatanga kutafuta ufumbuzi?. Kutokuamini ni dhambi na kunakukosesha majibu ya mahitaji magumu ya moyo wako. Mungu hashindwi na neno lolote.



Ushuda wa kweli : Umetokea katika nyanda za juu kusini mwa Tanzania.
Mama mmoja alikuwa na tatizo katika  kizazi, akafanyiwa upasuaji wa kukiondoa. Hakuwa amejaliwa mtoto yeyote. Alihuzunika sana kukosa mtoto. Akaamua kumwamini Mungu atendaye miujiza kupita fahamu za kibinadamu. Akatamka nitazaa mtoto kwa tumbo langu na kumnyonyesha kwa matiti yangu. Madaktari walimkanusha na watu wakamdhihaki. Muda si mrefu akayaona anabadilika , miezi tisa akazalishwa mtoto mzuri na daktari yuleyule aliyeondoa tumbo la uzazi. Mungu ni wa kushangaza ndiyo sababu anaitwa MUNGU anafanya njia pasipo na njia.

Alimpa mtoto mama asiye na tumbo la uzazi, atakosaje wewe mtoto uliye na tumbo? muujiza ni wako wewe, gharama ni imani ya kweli kwa Yesu , anakwambia,” Yote yawezekana kwake aaminiye.”

Rev. Mwl. F.M.Swenya
Mawasiliano:
 +255 67 469 595, 0784 469 595
     Email: swenyaflorian@gmail.com
Axact

Axact

Vestibulum bibendum felis sit amet dolor auctor molestie. In dignissim eget nibh id dapibus. Fusce et suscipit orci. Aliquam sit amet urna lorem. Duis eu imperdiet nunc, non imperdiet libero.

Post A Comment:

0 comments: