Wakristo wengi ni wepesi wa kwenda mbele za Mungu kupeleka Maombi, Dua na Sala zao kwa BWANA, ila si wepesi wa kupokea toka kwa Mungu.
Wanaamini Mungu anayakubali na kuyapokea maombi yao, sala na dua ila hawana UHAKIKA KAMA MUNGU AMEJIBU AU LA! Wengi wanaishia kubahatisha…Ni kama wanajaribu labda uenda BWANA YESU atawapa kile walichoomba.
Ila hili si tatizo la kizazi hiki cha WAAMINI, Lipo tangu zamani kabisa…leo ninayo mifano miwili…ebu jifunze pamoja nami;


1.ZEKARIA BABA YAKE YOHANA MBATIZAJI
Huyu alikuwa KUHANI (Mtumishi wa Madhabahuni) kama mimi, ambaye alikuwa na uhakika na NGUVU NA UWEZA wa Mungu katika kujibu na kushughulikia mahitaji na haja za watoto wake! Maana kila mara alikwenda PATAKATIFU PA PATAKATIFU kupeleka haja, mahitaji na maombi ya Watu wa Israel (Luka 1:5)
Kwa hiyo tangu ujana wake alikwisha dhibitisha ya kuwa Mungu yu hai na ni halisi na anajibu maombi…Hakuwa mgeni kuhusu tabia ya Mungu kujibu maombi.
Lakini cha ajabu, kuna wakati yeye mwenyewe aliwahi kuomba kwa Mungu ili ampe mtoto, maana mkewe alikuwa tasa (Luka 1:6) lakini Mungu alipoleta jibu kupitia kinywa cha malaika Gabrieli, Mzee Zekaria alianza KUUFUTA MUUJIZA WAKE…Hata ikambidi Malaika Gabriel amfunge mdomo [awe bubu kwa muda wote wa mimba ya Yohana Mbatizaji] ili asije akaufuta ule Muujiza (Soma Luka sura ya kwanza utagundua jambo hili, na utapata ufunuo huu)
Kama alivyofanya Zekaria, wengi wetu pia tuna tatizo la kuibatilisha miujiza yetu…Mungu anapotuma majibu ya maombi yetu, anatukuta tukiwa busy na KUTOAMINI kwingi mioyoni mwetu na MANENO YALIYO KINYUME NA KILE TULICHOOMBA NA KUUBATILISHA MUUJIZA HUSIKA…Kwa Zekaria alipata neema ya kufungwa kinywa ili muujiza ukae, wewe unaye Roho Mtakatifu na Neno la Mungu…Umalizapo kuomba, usiruhusu Maneno na mawazo yaliyo kinyume na Ulichokiri wakati wa maombi mbele za BWANA!
TUMBO LA MTU HUSHIBA MATUNDA YA MIDOMO YAKE (Mithali 18:20-21)
TUNZA MUUJIZA WAKO MARA BAADA YA MAOMBI USIRUHUSU MANENO YAKO YANAYOANGALIA KILE KILICHOKUZUNGUKA KUHARIBU MUUJIZA WAKO…Kumbuka, “Tunaenenda kwa Imani na si kwa kuona” (2Kor 5:7)!

MITUME; PETRO ALIPOFUNGWA
Ukisoma Matendo 12 yote, utaona tukio hili…
Kuna wakati Mfalme Herode alimuua Yakobo, na kisha akamweka Petro Gerezani.
Na Biblia inasema KANISA likamwomba Mungu kwa ajili yake (Matendo 12:5)
Kumbuka: Hawa walikuwa Mitume, ambao Mungu aliwatumia kutenda Ishara, maajabu na Miujiza Mikubwa. Na hapa walipatana ya kuwa watakesha usiku kucha wakimwomba Mungu ili amtoe Petro gerezani naye asiuwawe kama Yakobo.
Biblia inasema Mungu aliyasikia maombi yao, na usiku wa manane, Mungu alimtuma Malaika wake akaenda mle gerezani akamtoa Petro na kumpeleka hadi pale wale Mitume [kanisa] WALIPOKUWA WAKIENDELEA KUOMBA…
Kijakazi akasikia mlango ukigongwa, akaenda kusikiliza ni nani anayegonga…alipofika na kugundua kuwa ni Petro, alirudi bila kumfungulia mlango, akawanyamazisha wale WAOMBAJI na kuwaambia Petro yuko pale nje anagonga…KWA LUGHA NYINGINE ALIKUWA ANAWAAMBIA, “ACHENI KUOMBA, MAOMBI YAMEJIBIWAAAA, YESU AMETENDA…”
Cha kushangaza, badala ya wale ndugu kuungana na huyu kijakazi kumshukuru na kumtukuza Mungu kwa kujibu maombi yao, wao walimgeukia kwa pamoja na wakamwambia, “WEWE VIPI? UNA WAZIMU NINI? PETRO ANAGONGA? HAIWEZEKANI? ACHA TUOMBE HADI ASUBUHI, MUNGU ATATENDA…UMETUKATISHA MAOMBI YETU…UMEUKATA UWEPO WA MUNGU, TENA SIKU NYINGINE USIRUDIE…” (Hapa nimeweka msisitizo kama Mwalimu)
Kwa kweli inashangaza…inaonesha waliamua kuomba KAMA KUJARIBU HIVI…au WALITEGEMEA MUNGU ATAMTOA PETRO KWA NJIA WANAZOJUA WAO…WALIJARIBU KUFIKIRIA KWA JINSI YA KIBINADAMU (Kama wewe unavyajaribu kumpangia Mungu namna ya kukusaidia au kushughulikia mahitaji yako; acha utoto, USIMWEKEE MUNGU WANGU MIPAKA; HE IS OMNISCIENT, OMNI PRESENT and OMNIPOTENT…Mawazo yake na njia zake ziko juu sana, na hazichunguziki: Isaya 55:8-11)


MUHIMU:
Unapoingia mbele za Mungu kuomba, ukiwa na uhakika ya kuwa kile unachokiomba kiko sawa na Mapenzi ya Mungu (NENO LAKE) uwe na uhakika ya kuwa Mungu amekusikia sekunde hiyohiyo, na kama amekusikia, tayari unazo haja zote ulizomwomba (1Yohana 5:14-15)
Yesu alisema, “YEYOTE ATAKAYEUAMBIA MLIMA HUU NGOKA NA UJITOSE BAHARINI, WALA ASIONE SHAKA MOYONI MWAKE, BALI AAMINI YA KUWA YALE ALIYOSEMA YAMETUKIA [sio yatatukia bali yametukia] YATAKUWA YAKE” (Marko 11:23)
KUOMBA SI KAZI, KAZI NI KUPOKEA YALE UYAOMBAYO…ACHA KUOMBA, POKEA MAJIBU YA MAOMBI YAKO SASA!
Axact

Axact

Vestibulum bibendum felis sit amet dolor auctor molestie. In dignissim eget nibh id dapibus. Fusce et suscipit orci. Aliquam sit amet urna lorem. Duis eu imperdiet nunc, non imperdiet libero.

Post A Comment:

1 comments:

  1. Amina kubwa barikiwa sana mtumishi wa mungu,hakika mungu ni mkuu na anatenda na kujibu kwa wakati alioupanga

    JibuFuta