Counselor Nicholaus

UTANGULIZI.
 Ni maombi yangu kwako, Mungu afungue ufahamu wako uweze kupata maarifa haya, ambayo yawe msaada kwako binafsi na jamii inayo kuzunguka..
Amen.
MAELEZO YA DARASA HILI LA USHAURI.
Darasa hili nimeliandaa, kwaajili ya kutoa utangulizi wa elimu ya ushauri juu ya kujua kanuni za msingi na mbinu za kushauri zilizo bora.
MAKUSUDI YA DARASA HILI.
Ni kutoa fursa kwa watu mbalimbali wenye wito na huduma hii, Waweze kujifunza mbinu za msingi za kutumia katika kushauri kwa kiwango kizuri pasipo ubabaishaji.
MALENGO YA DARASA HILI.
1. Kupata uelewa wa Msingi wa maana ya ushuri.
2. kupata uelewa wa msingi wa mbinu za kusaidia wakati wa kushauri.
3. kubadilisha mtizamo wa watu juu ya elimu ya ushuri.

MAHITAJI YA DARASA.
1. Ushiriki wako kikamilifu kwa kufatilia vipindi vyote.
2. kijarida cha kuandikia. Hiki kitakusaidia kuandika baadhi ya vitu vya muhimu kwako.

SEHEMU YA KWANZA

       UMUHIMU WA ELIMU YA USHAURI
          1. Elimu ya ushauri huliponya taifa na kuleta msaada mkubwa.
       2. Ushauri unasaidia kupambana na mambo yasiyofaa na kuleta wokovu katika maisha ya mwanadamu.
          3. Ushauri unaleta njia ya kutokea.
          4. Wanaotafuta ushauri, hupata amani na furaha.
         5. Mshauri akitoa ushauri mbaya usiojenga afanya machukizo mbele za Mungu.

Unapokuwa unahitaji msaada wakati wa shida, kuchanganyikiwa, tunapaswa kutumia maneno yenye hekima ya Ki-Mungu ndani yake kwasababu Mungu ndiye mshauri wetu, kwa urahisi kabisa kushauri ni kule kutembea katika misingi iliyo sahii chini ya uongozi wa Mungu, pasipo Mungu kuhusika katika ushauri wowote, matokeo yake huwa siyo mazuri..

Ushauri ni  nini?
Ni matumizi ya ujuzi ulionao kwa makusudi kuwasaidia watu wengine kuweza kugundua na kutekeleza masuluhisho katika matatizo yao. (Manthei, 1997)
Ni mchakato  ambao unajumuisha majibizano kati ya mshauri na mshauriwa katika sehemu  maalum kwa nia ya kumsaidia mshauri kabadili tabia yake ili kuweza kupatikana  suluhisho la kutosheleza linalohitajika.
-katika  mazungumzo haya, mshauriwa anapaswa kujihisi yuko salama. .
Kwasababu kushauri huwa inarejea katika utaratibu wa kuwasaidia watu waweze kutatua matatizo yao wenyewe.
Ushauri huwa unawasaidia watu kuhakikisha kuwa wanafikia mafanikio yao binafsi (kwa lengo la kuweza kumudu maisha yao ya baadae). Kwahiyo, mshauri anapaswa kuwa na ujuzi unaotakiwa.

Ni mimi ndugu yako counselor Nicholaus Simon.
Kwa msaada zaidi na ushauri.
whatsap: 0654-623492
pataufahamu@gmail.com
Ubarikiwe sana Na nakuomba nisaidie kushare kwa marafiki zako ili wao wajifunze.

Axact

Axact

Vestibulum bibendum felis sit amet dolor auctor molestie. In dignissim eget nibh id dapibus. Fusce et suscipit orci. Aliquam sit amet urna lorem. Duis eu imperdiet nunc, non imperdiet libero.

Post A Comment:

0 comments: