@Ujana wenye matokeo

A. KIMWILI
Wimbo 2:7, 8:4.(NEN)
“Binti za Yerusalemu, ninawaagiza kwa paa na kwa ayala wa shambani: Msichochee wala kuamsha mapenzi hata yatakapotaka yenyewe.”
"Binti za Yerusalemu, ninawaagiza: msichochee wala kuamsha mapenzi hata yatakapotaka yenyewe."

MUHIMU: 
Katika ujana, changamoto kuu ni kuyaamsha/kuchochea mapenzi kabla ya wakati wake”

Fahamu mambo kadhaa yanayo sababisha hali hiyo:-
Jambo la kufahamu ni kwamba Mungu ameweka wakati maalumu kwa kila jambo.
Mhubiri 3:1“Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.”

MAMBO YANAYOWEZA KUAMSHA/KUCHOCHEA MAPENZI KABLA YA WAKATI
1   1. Maongezi Mabaya. 
1Kor 15:33,“Msidanganyike; Mazungumzo mabaya huharibu tabia njema.”
 1Tim 4:7 “Bali hadithi za kizee, zisizokuwa za dini, uzikatae; nawe ujizoeze kupata utauwa.”
2Tim 2:16a,23 “Jiepushe na maneno yasiyo na maana, ambayo si ya dini; kwa kuwa wataendelea zaidi katika maovu,Walakini uyakatae maswali ya upumbavu yasiyo na elimu, ukijua ya kuwa huzaa magomvi.”
Maneno yasiyofaa yana mchango mkubwa kumpeleka kijana sehemu isiyofaa, vijana leo;unaweza kukuta wanawajadili wanawake mfano mguu, sura za wadada/wakaka.

2. Nyimbo za kidunia/tamthilia za mapenzi. 
Mithali 4:23, “Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo; Maana ndiko zitokako chemchemi za uzima.”, “Be careful how you think;your life is shaped by your thoughts. (Today English Version)” 
Rumi 12:2,  “Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.”
“Do not conform to the pattern of this world, but be transformed by the renewing of your mind. Then you will be able to test and approve what God’s will is—his good, pleasing and perfect will. New International Version (NIV)”

Elewa kuwa nyimbo yoyote/mziki ina mambo makubwa 3
i.                 Ina nguvu na uwezo wa kuathiri nafsi,moyo/roho(vinaweza kujazwa furaha au huzuni)

ii.                  Ina uwezo wa kuathiri hisia zako na kukuumbia tabia Fulani/roho Fulani.

iii.                Ipo nguvu ya kuponya/kuharibu

3. Kuzoeana kupita kiasi/ukaribu
Hii ni hatari mfano, kijana wa kike na wakiume kutembeleana tena wakiwa wawili.
Efeso 5:15-16, “Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima; mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu.”

     4. Mizaha kupita kiasi kati ya jinsia mbili tofauti.
        Zaburi 1:1c, “Heri mtu yule asiyekwenda Katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.”
Mizaha ni matendo ya masihara,kejeli,au ukosefu wa umakini katika kufanya au kusema jambo, mfano eti kijana wa kiume anataniana na binti eti wahi nyumbani Mama ukanipikie chakula basi.

      5. Picha za ngono. 
       Ayubu 31:1,“ Nilifanya agano na macho yangu; Basi nawezaje kumwangalia msichana?”
      2kor 7:1,“Basi, wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo, na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha Mungu.”
Hizi zimechangia hata hali ya kumpenda Mungu imeshuka, ufaulu mashuleni umeshuka na pia kupelekea Vijana kujiingiza kwenye maswala ya upigaji punyeto(musterbation), na kwa mabinti hali ya kujichua.
Hii hupelekea madhara makubwa katika ndoa.

   6. Marafiki wabaya. 
Mithali 13:20,“Enenda pamoja na wenye hekima, nawe utakuwa na hekima; Bali rafiki wa wapumbavu ataumia.”
Iko nguvu kubwa ya kuathiriana kati ya Rafiki na Rafiki. Hivyo ni muhimu kuwa mwangalifu na aina ya Rafiki uliye naye. Je,ana manufaa yoyote kwako?

       7. Mavazi ya kikahaba
      Mithali 7:10, Na tazama, mwanamke akamkuta, Ana mavazi ya kikahaba, mwerevu wa moyo;
Mavazi yanamchango mkubwa sana katika kuchochea mapenzi kwa vijana. Mfano kwa kijana wa kiume yapo maeneo hatari sana akiyaona kwa binti mfano: Mapaja ya binti, matiti, makalio n.k
Ieleweke kwamba kijana wa kiume hisia zake huongozwa kwa macho, na hivyo mara nyingi macho yake anapokutana na binti huanza kumwangalia sehemu ya kifuani(kisaikolojia)

      8. Kutokuwa na mipaka ya kupigiana simu 
       2Tim 2:16a,23 ”Jiepushe na maneno yasiyo na maana, ambayo si ya dini; kwa kuwa wataendelea zaidi katika maovu,Walakini uyakatae maswali ya upumbavu yasiyo na elimu, ukijua ya kuwa huzaa magomvi.”
Mfano: kijana wa kike na wakiume wanapigiana simu saa tano au saa sita, alafu kwa kuwa hawana cha maana cha kuzungumza, wanaanza kuulizana mfano:umelalaje muda huu? Chali au kifudifudi? Unasikia baridi? umevaa nini? Haya yote huchochea hali ya ndani sana ya hisia za mapenzi na kujikuta vijana wengi kufanya uasherati.
                         "Youth’s Pastor: Fred Mwabulambo (TAG ICC LUGALO) 0752 156 304"

    Ni mimi ndugu yako; Mwl Nicholaus Simon.
    Kiungo katika mwili wa kristo.
    Kwa msaada zaidi na ushauri. 
    Mawasiliano: +255 766 635 382
    pataufahamu@gmail.com

    Ubarikiwe sana Na nakuomba nisaidie kuishare kwa marafiki zako ili na wao wajifunze Neno la Mungu.

Somo letu litaendelea.....

Axact

Axact

Vestibulum bibendum felis sit amet dolor auctor molestie. In dignissim eget nibh id dapibus. Fusce et suscipit orci. Aliquam sit amet urna lorem. Duis eu imperdiet nunc, non imperdiet libero.

Post A Comment:

0 comments: